Kujenga Afrika Mashariki yenye mshikamano, maendeleo ya pamoja, na vijana wenye uwezo wa kiuchumi na kijamii.
Jessica Mshama ni mjasiriamali na kiongozi wa vijana kutoka Tanzania, anayejikita katika kukuza elimu ya kidijitali, uwezeshaji wa kiuchumi na maendeleo ya vijana lakini pia Jessica Mshama ni Mjumbe wa Bodi wa Their Story Is Our Story (TSOS), shirika la kimataifa linalojikita katika kusimulia hadithi za wakimbizi, kukuza huruma, na kushawishi sera zinazounga mkono jamii zilizolazimika kuhama makazi yao duniani kote.. Alisoma masuala ya biashara na fedha katika Catholic University of Eastern Africa, Nairobi. Licha ya wazazi wake kumtia moyo kusoma nje ya nchi, alichagua kurejea Tanzania baada ya masomo yake kwa lengo la kuchangia maendeleo ya jamii na kuunda fursa za kijamii na kiuchumi kwa vijana.
Falsafa ya Maisha: Ujuzi wa kidijitali na elimu ni msingi wa kujenga jamii yenye usawa na fursa sawa. Anaamini kuwa vijana wenye ujuzi wa teknolojia wana uwezo wa kuleta mageuzi.
DIRA YA UONGOZI: Kujenga Afrika Mashariki yenye mshikamano, maendeleo ya pamoja, na vijana wenye uwezo wa kiuchumi na kijamii kupitia sera bunifu, teknolojia, na ushirikiano wa kikanda.
Jessica ni mjumbe wa Bodi ya Utendaji ya NAMYO, anachangia kupanga mwelekeo wa kimkakati, akitetea maslahi ya vijana kutoka nchi zisizofungamana na upande wowote. Makao makuu Azerbaijan, matawi nchi 93 duniani, chini ya Wizara ya Mambo ya nje ya Azerbaijan. Pia ni mwakilishi wa Bodi ya Kimataifa anayei wakilisha Afrika.
Uthibitisho wa Kimataifa: Cheti cha Ushiriki kama Mtaalamu (Expert) – International Youth Forum of Public Diplomacy InterYES! 3.0, na Commonwealth Youth Forum 2024.
"Kujenga kizazi chenye ujuzi wa kidijitali, uwajibikaji na uwezo wa kujitegemea kiuchumi – kwa Afrika tuliyotaka. Ninaamini katika nguvu ya vijana kuleta mageuzi."
Jessica Mshama | Balozi wa Vijana EAC · Mjumbe Bodi NAMYO · Mgombea Ubunge EAC
© 2026 | Jessica Mshama — portifolio Identity System